
Shuhuda wa tukio hilo amedai kwamba majira ya mchana kweupe gari aina ya Toyota Mark X lenye rangi nyeusi liliwasili kwenye viunga vya hoteli hiyo na kusimama kwa takribani dakika 10 kisha likaondoka na kwenda kupaki sehemu nyingine ambapo ni umbali mfupi toka hotelini hapo...

"Walipoondoka na kupaki palipojificha tuliamua kuwasogelea ili tujue ni akina nani
"Baada ya muda, kioo cha dereva kilishushwa kidogo, tukamuona dogo anayefanana na Diamond akiwa anampapasa demu aliyekuwa pembeni yake...
"Tulipoona hivyo, tulidhana mnyamwezi ameamua kumaliza mambo yake ndani ya gari, hivyo tukaziweka simu zetu standby kwa ajili ya kushuhudia" alisema shuhuda huyo
Baada ya muda, mlango wa kulia ulifunguliwa kisha wakamuona dogo aliyetambuliwa kwa jina la Nasry
"Kumbe hakuwa Diamond,alikuwa ni dogo Nasry.Tulipotupa jicho ndani, tulihamaki kumuona Rose Ndauka akibadili nguo na kujitanda baibui.
"Nadhani alifanya hivyo ili watu wasimjue pindi atakaposhuka kwenye gari maana aliposhuka tu, waliongozana na dogo Nasry kwa mwendo wa kasi hadi ndani...

0 maoni:
Post a Comment